Watanzania wamepewa Tahadhari dhidi ya ugonjwa wa chikunganya - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!

Friday, 19 January 2018

Watanzania wamepewa Tahadhari dhidi ya ugonjwa wa chikunganya

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa tahadhari kuhusu ugonjwa wa homa ya Chikuganya ambao umeripotiwa na vyombo vya habari kutokea jijini Mombasa nchini Kenya.


Taarifa iliyotolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu imesema kuwa mpaka sasa Shirika la Afya Duniani (WHO) bado haijatoa taarifa rasmi lakini wao wanaotoa taadhari kuzingatia muingiliano mkubwa wa watu baina ya nchini hizi mbili Kenya na Tanzania. 

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya wanasema kuwa ugonjwa wa Chikunganya unasababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa mbu wa aina ya Aedes na kusema ugonjwa huu si mgeni nchini Tanzania kwani ulishawahi kutokea

No comments:

Post a Comment