Mattembe ametoa wito huo wakati alipokuwa akiwahamasisha wananchi wa Kata ya Ilongero kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ikiwa imebaki siku moja tu ya kujiandikisha.
Alisema maendeleo ya nchi yanaanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, kata, wilaya hadi Taifa hivyo tiketi ya kuweza kuchagua kiongozi mwenye sifa nilazima kwenda kujiandikisha ili kumchagua kiongozi anayefaa.
"Bila ya kujiandikisha haitawezekana kumchagua kiongozi mnaye mtaka hivyo wito wangu kwenu kwa hii siku moja iliyobaki kwa ajili ya kujiandikisha jitokezeni kwa wingi vinginevyo mtapoteza haki yenu ya kumchagua kiongozi mnaye mtaka” alisema Mattembe.
Aliwataka wananchi hao kujitokeza kujiandikisha bila kujali itikadi ya vyama vyao kwani maendeleo hayana chama yapo kwa ajili ya watu wote.
No comments:
Post a Comment