Hitimana Thierry amtabiria Pablo Franco - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Thursday, 11 November 2021

Hitimana Thierry amtabiria Pablo Franco

 


Aliyekuwa Kocha Mkuu wa muda wa klabu ya Simba, Hitimana Thierry ametoa neno kuhusu ujio wa kocha mpya wa klabu hiyo, Mhispania Pablo Franco na kusema ana imani kocha huyo ataivusha Simba kwenye kipindi kigumu kinachoipitia hivi sasa.


Hitimana amesema, “Nimefurahi kukutana naye naamini huu ni wakati wa kumpa muda na ushirikiano ili aweze kuitoa Simba mahala ilipo na kuipeleka mbele zaidi kama alivyofanya mtangulizi wake”. 


Hitimana ameyasema hayo kocha mpya wa Simba, Pablo Franco alipowasili nchini Novemba 10, 2021 na kutembelea kambi ya wachezaji na Uongozi wa klabu hiyo maeneo ya Bunju pembeni kidogo mwa jiji la Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here