Maafisa katika mji mkuu wa Afghanistan Kabul, wanasema wamemaliza mkwamo wa saa 12 kufuatia shambulio la wanamgambo dhidi ya hoteli kubwa ya Intercontinental. Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani amesema raia wasita wameuawa, pamoja na washambuliaji wote watatu. Ni ishara ya hivi karibuni ya ghasia zinazoendelea kushudiwa nchini Afghanistan. Usiku kucha, vikosi maalum vilipambana kuidhibiti hoteli hiyo. Zaidi ya watu 150, wakiwemo wageni, walikuwemo ndani ya hoteli hiyo Jumamosi jioni wakati washambuliaji waliojihami kwa bunduki walipoivamia hoteli hiyo na kuanza kufyetuwa risasi. Televisheni nchini humo zimewaonyesha wageni wakishuka kutoka orofani kwa kutumia matandiko, waliyoyafunga kwenye roshani na kukwepa. Picha ya maktaba: The Intercontinental Hotel, picha iliyopigwa Januari 2016Haki miliki ya pichaREUTERS Image caption Picha ya maktaba: The Intercontinental Hotel, picha iliyopigwa Januari 2016 Moshi mkubwa ulitanda usiku angani, ikiwa ni baada ya sehemu ya jengo hilo kuteketezwa moto. Hoteli hiyo ya Intercontinental ni mojawapo ya majengo makuu ya mji wa Kabul. Hutumika sana na wageni wa nchi za nje, wanasiasa nchini, hutumika pia kuandaa shrehe za harusi na mikutano. Ni eneo la wazi linaloweza kulengwa na wanamgambo na lilishambuliwana wapiganaji wa Taliban miaka 7 iliyopita. Ramani ya Afghanistan Image caption Ramani ya Afghanistan Lakini shambulio hili la sasa lililodumu kwa muda mrefu na linaloonekana kuwa gumu, linajiri katika wakati ambapo kuna ongezeko la wasiwasi kuhusu kudorora kwa usalama katika mji mkuu huo, na litazusha maswali kuhusu vipi usalama wa kivitengo katika hoteli hiyo ulivyoweza kuvukwa. - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Sunday, 21 January 2018

Maafisa katika mji mkuu wa Afghanistan Kabul, wanasema wamemaliza mkwamo wa saa 12 kufuatia shambulio la wanamgambo dhidi ya hoteli kubwa ya Intercontinental. Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani amesema raia wasita wameuawa, pamoja na washambuliaji wote watatu. Ni ishara ya hivi karibuni ya ghasia zinazoendelea kushudiwa nchini Afghanistan. Usiku kucha, vikosi maalum vilipambana kuidhibiti hoteli hiyo. Zaidi ya watu 150, wakiwemo wageni, walikuwemo ndani ya hoteli hiyo Jumamosi jioni wakati washambuliaji waliojihami kwa bunduki walipoivamia hoteli hiyo na kuanza kufyetuwa risasi. Televisheni nchini humo zimewaonyesha wageni wakishuka kutoka orofani kwa kutumia matandiko, waliyoyafunga kwenye roshani na kukwepa. Picha ya maktaba: The Intercontinental Hotel, picha iliyopigwa Januari 2016Haki miliki ya pichaREUTERS Image caption Picha ya maktaba: The Intercontinental Hotel, picha iliyopigwa Januari 2016 Moshi mkubwa ulitanda usiku angani, ikiwa ni baada ya sehemu ya jengo hilo kuteketezwa moto. Hoteli hiyo ya Intercontinental ni mojawapo ya majengo makuu ya mji wa Kabul. Hutumika sana na wageni wa nchi za nje, wanasiasa nchini, hutumika pia kuandaa shrehe za harusi na mikutano. Ni eneo la wazi linaloweza kulengwa na wanamgambo na lilishambuliwana wapiganaji wa Taliban miaka 7 iliyopita. Ramani ya Afghanistan Image caption Ramani ya Afghanistan Lakini shambulio hili la sasa lililodumu kwa muda mrefu na linaloonekana kuwa gumu, linajiri katika wakati ambapo kuna ongezeko la wasiwasi kuhusu kudorora kwa usalama katika mji mkuu huo, na litazusha maswali kuhusu vipi usalama wa kivitengo katika hoteli hiyo ulivyoweza kuvukwa.

Vikosi vya Afghan vyatibua shambulio katika hoteli Kabul


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here