Aliyemuua Mwanamuziki Radio ahukumiwa miaka 14 Jela - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Thursday, 31 October 2019

Aliyemuua Mwanamuziki Radio ahukumiwa miaka 14 Jela



Mahakama Kuu nchini Uganda imemuhukumu kifungo cha miaka 14 jela Godfrey Wamala maarufu Troy kwa kosa kumuua mwanamuziki Moses Ssekibogo maarufu Mowzey Radio. Troy alipatikana na hatia siku ya Jumatatu

Radio alifariki Februari 1, 2019 baada ya kupigana na Troy wakiwa baa mwaka jana.

Godfrey Wamala amekutwa na hatia ya kumuua Moses Sekibogo (Mowzey Radio) bila ya kukusudia. Hukumu hiyo imesomwa licha ya Mwanamuziki huyo kufariki katika ghasia zilizotokea sehemu ya starehe

Kesi ilikuwa ikiendeshwa na Jaji Jane Abodo katika Mahakama Kuu Entebbe, Jaji amesema kuwa Godfrey Wamala atatumikia miaka 13, miezi 3 na siku 4 baada ya kukaa mahabusu kwa mwaka mmoja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here