Mashindano ya siku ya Takwimu Afrika kuanza Novemba 2 - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!

Thursday, 31 October 2019

Mashindano ya siku ya Takwimu Afrika kuanza Novemba 2



Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar imeandaa mashindano maalum la michezo wa soka la kuvuta kamba yatakayoanza Novemba 2 mwaka huu.

Mashindano hayo yatakayoshirikisha baadhi ya wizara za serikali na mashirika, yatafanyika katika kiwanja cha Mao Zedong na fainali ya michezo hiyo itapigwa kati ya Novemba 16 au 17.

Mratibu wa mashindano hayo Abdalla Mawazo, amesema timu sita zitashiriki na zimepangwa katika makundi mawili. Amezitaja timu zitakazoshiriki kwa michezo yote kundi A Mkaguzi wa Hesabu, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Biashara, wakati kundi B litakuwa na timu za Bodi ya Mapato ZRB, Wizara ya Wanawake na Watoto na Mamlaka ya Manunuzi.

No comments:

Post a Comment