Na: Mchungaji Daniel Ntebi
NENO: WAEFESO 4:7-14, YOEL 2:28
KUSUDI: KUMWEZESHA KILA MKRISTO AFAHAMU
KWA KIASI KUHUSU KARAMA YAKE MWENYEWE NA KUMHAMASISHA AITUMIE KWA USTAWI WA
KANISA.
MAMBO YA MSINGI TUTAKAYOYATAZAMA.
·
Utangulizi.
·
Maana ya Karama.
·
Orodha ya Karama.
·
Kwanini Mungu alitoa
Karama.
·
Kutambua, kukuza na kutumia
Karama.
·
Karama zinazotumika isivyo
Kanisani.
·
Kustawisha Karama Kanisa.
1. UTANGULIZI.
Mungu
amemimina Roho Mtakatifu kwa kila Mkristo. Hivyo, Mungu anatarajia kuona Karama
au vipawa mbalimbali katika Kanisa. Kanisa likikosa Karama ni sawa na mtu aliye
hai lakini ni mgonjwa tabani. Hii hupelekea Kanisa kuwa dhaifu sana. Karama zikitumika
Kanisa ipasavyo, Kanisa litakuwa hai a lenye afya kamili.
2. MAANA
YA KARAMA.
-
Karama ni zawadi anayopewa
Mkristo baada ya kuamini kama nyenzo ya kutumika katika kuutangaza ufalme wa Mungu.
-
Kipawa ni uwezo anaozaliwa
nao mtu kumsaidia katika Maisha yake anapoishi na jamii inayomzunguka.
Kwaiyo, Karama inamilikiwa na Mkristo tu, bali Kipawa anaweza
kuwa nacho mtu yeyote. Kipawa cha mtu aliyeokoka hugeuka na kuwa Karama. Wakati
mwingine maneno haya mawili yanaweza kutumika kwa Mkristo kama neno moja linalofanana.
Efeso 4:8 “Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa”.
-
Kuna tofauti kati ya
‘Karama’ na ‘Tunda la Roho Mtakatifu’;
a. Karama
huonyesha mtu anachofanya.
-
Mfano; ni kufundishana na
kuonyana n.k.
b. Tunda
La Roho Mtakatifu huonyesha jinsi mtu alivyo. Wagalatia 5:22,23 “Lakini tunda
la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhli, uaminifu, upole,
kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sharia”.
-
Mfano; ni upendo, upole, uvumilivu
n.k.
3. ORODHA
YA KARAMA.
- 1 Korintho 12, Warumi 12, Waefeso 4.
a. Unabii
b. Huduma
c.
Kufundishana
d. Kuonyana
e. Kukirimu
f.
Kusimamia
g. Kurehemu
h. Hekima
i.
Maarifa
j.
Imani
k. Kuponya
l.
Miujiza
m. Kupambanua
Roho
n. Aina
za Lugha
o. Tafsiri
za Lugha
p. Utawala
q. Useja
– 1 Korintho 7:7 “Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo;
walakini kila mtu ana Karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu
hivi”.
4. KWANINI
MUNGU ALITOA KARAMA?
a. Ili
Mungu atukuzwe.
1 Petro 4:10,11 “Kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana;
kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu
akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika
mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele.
Amina.”
Ø Karama zte zimelenga kumtukuza Mungu peke yake
b. Ili
wakristo wapate kufaidiana.
Kila mkristo anahitaji kufaidika na baraka za Mungu kwa
njia ya Karama mbalimbali. Kwa mfano; uponyaji n.k. 1 Korintho 12:7 “Lakini
kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.”
c.
Ili kuujenga mwili wa Kristo.
Kanisa linafananishwa na nyumba inayojengwa mpaka ikamilike
au ifikie kiwango kinachotakiwa.
1
Korintho 14:26 “Basi ndugu imekuaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi,
ana fundisho, ana ufunuo, ana Lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kw kusudi
la kujenga.”
Waefeso 4:12 “Kwa kusudi la kuwakamilisha
watakatifu, hata kazi ya Huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe.”
5. I.
KUTAMBUA KARAMA YAKO
Wakristo wengi hawafahamu
karama zao. Zifuatazo ni njia zitakazomsaidia mkristo kutambua Karama yake:-
a. Tafakari
moyo wako unakusukuma kufanya nini kaanisani? Msukumo huu huwa hautulii.
Yeremia 20:9 “Nami nikisema, sitamtaja, wala sitasema
tena kwa jina lake; basi, ndipo moyoni mwangu kumekuwamo kama moto uwakao, uliofungwa
ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kustahimili, wala siwezi kujizuia.”
b. Ukifanya
hilo jambo unajisikiaje au usipolifanya unajisikiaje?
Ukiifanya Karama yako lazima ujisikie vizuri na usipoifanya
utajisikia vibaya. 1 Korintho 9:16 Maana, japo kuwa naihubiri injili, sina
la kujisifia; maana nimeweka sharti; tena ole wangu nisipoihubiri injili.”
c.
Je, watu wanamwitikio gani
kwa Huduma yako?
Ø
Wanaweza kufurahi. Matendo
21:17 “Tulipofika Yerusalemu ndugu wakatukaribisha kwa furaha.”
Ø Hata
hivyo, kumbuka shetani yumo kazini anaweza kukukatisha tamaa. Matendo 16:16
“Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na
pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.”
II. KUKUZA KARAMA
YAKO.
Karama hukua kwa kila mkristo. Yapo mambo ya
kuzingatia ili kukuza Karama yako.
a. Omba
Mungu aikuze Karama yako. Waefeso 9:19 “Pia, na kwa ajili yangu mimi, nipewe
usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya injili.”
b. Soma
Neno la Mungu litaikuza Karama yako.
2 Timotheo 4:13 “Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko
Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya Ngozi.”
c.
Kaa karibu na kiongozi wako,
atakuelekeza ili ukue. Yesu naye alikaa na mitume.
Matendo 15:39 “Basi palitoke mashindano baina yao hata
wakatengana. Barnaba akamchukua marko akatweka kwenda Kipro. Linganisha
na 2 Timotheo 4:11 “Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae
Marko, umlete pamoja nawe, maana ananifaa kwa utumishi.
d. Jifunze
Neno la Mungu kutoka vyanzo sahihi. Mfano kuhudhuria semina, makongamano, ibadani n.k. Waefeso
4:11-12 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine
kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na walimu; kwa kusudi la kuwakamilisha
watakatifu, hata kazi ya Huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe.”
III. KUTUMIA KARAMA
YAKO.
a. Tumia
Karama yako kwa ustawi wa Kanisa. 1 Wakorintho 12:7 “Lakini kila mmoja hupewa
ufunuo wa Roho kwa kufaidiana”. Kila Mkristo amapewa Karama hiyo
kwa ustawi wa Kanisa. Mkristo anaelalia Karama yake ana lengo la kudhoofisha Kanisa.
b. Mkristo
anayetumia Karama yake atapata thawabu siku ya mwisho. Daniel 12:3 “Na walio
na Hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa
kama nyota milele na milele”.
c. Mkristo
aliyekalia Karama yake ataadhibiwa siku ya mwisho. Luka 12:47 “Na mtumwa
yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake,
atapigwa sana”.
6. KARAMA
ZINAZOTUMIKA ISIVYO KANISANI.
Kuna Karama chache ambazo
Kanisa la leo halizitumii ipasavyo:-
A. Kunena
kwa Lugha. 1 Wakorintho 14: 1-2 “Ufuateni upendo, na kutaka sana Karama
za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu. Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi
na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri
katika roho yake”. Makanisa ya kipentekoste yameitazama Karama hii
kuwa ni tofauti kabisa.
i.
Hulazimisha kila mtu anene
kwa lugha. Marko 16:17,18 “Na ishara hizi zitafuatana nao waaminio; kwa jina
langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu
cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata
afya”. Paulo analiweka sawa hili kuwa wote hawawezi kuwa na
Karama moja tu Kanisa; 1 Wakorintho 12: 8,9,30 “Maana mtu mmoja kwa Roho apewa
neno la Hekima; na mwingine neno ka maarifa, apendavyo Roho yeye yule; mwingine
Imani katika Roho yeye yule; na mwingine Karama za kuponya katika Roho yule mmoja;
wote wanakarama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?”.
ii.
Wapentekoste hulazimisha kunena
wakati wowote tu hata anahubiri au kuomba. Paulo anatoa utaratibu wanene wawili
au watatu, tena zamu kwa zamu ikiwa yupo wa kufasiri. 1 Wakorintho 14:27 “Kama mtu akinena
kwa lugha, wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue”. Kama
hayuko wa kufasiri Kanisani asitokee wa kunena kwa lugha. 1 Wakorintho 14:28 “Lakini asipokuwapo mwenye
kufasiri na anyamaze katika Kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu”.
B. Kutoa
Unabii. Unabii ni maneno yote ya Mungu aliyotuletea Mungu yaani maneno yote yaliyomo
katika Biblia. Nabii ni mtu yeyote aliyejaa Roho Mtakatifu anayepokea neno la Mungu
kulipeleka kwa watu. Agano la Kale Mungu alizungumza nasi kupitia manabii. Lakini
siku hizi Mungu amesema nasi kupitia mwanaye.
-
Robo tatu ya unabii wa
Biblia unaonya au unawahamasisha watu kuishi Maisha ya Mbinguni (forthtell)
na Robo inayobakia inazungumzia siku zijazo (foretell).
-
Kwa kuwa sasa Mungu amesema
kupitia mwana wake (Agano jipya), hakuna unabii mpya tunaweza kupata.
-
Kila mtu atayenena maneno
ya unabii (Biblia) lazima tumpime kama anasema sawa kama Waberoya walivyowapima
wahubiri. Yohana anasema tuzijaribu kila roho, maana wapo manabii wa uongo wadanganyao
watu. 1 Yohana 4:1-4 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho,
kwamba zimetoka na Mungu; kwa sababu manabiiwa uongo wengi wametokea duniani. Katika
hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika
mwili yatokana na Mungu. Kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndio
roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
Ninyi, Watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye
ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia”.
C. Uponyaji.
Karama hii imechezewa sana, kwani hata ushirikina umeingia ndani. Mfano; Ni vyema
kuwa makini na mtu aliyebeba Karama hii. Hata wengine wametoza watu fedha nyingi
kwa shida zo, jambo ambalo si sawa. Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni
wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.
7. KUSTAWISHA
KARAMA KANISANI.
Ili Kanisa listawi kabisa,
yafuatayo yazingatiwe:-
a. Viungo
vyote vya mwili vifanye kazi kwa ushirikiano. 1 Wakorintho 12:12-15 “Maana
kama vile mwili mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo
ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi
sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu wahayahudi au kwamba tu wayunani; ikiwa
tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. Kwa maana mwili
si kiungo kimoja, bali ni vingi. Mguu ukisema, kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa
mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo?”. Kwahiyo, kila mtu Kanisani
anatakiwa awajibike na Karama yake mfano, Mwalimu, Mwanasheria, Afisa rasilimali
watu, Fedha, Takwimu, IT, Mfanyabiashara, mwimbaji, Mshauri, Mwanatheorogia n.k,
kila kiungo/Karama lazima kiheshimiwe. Zaburi 133:1-3 “Tazama, jinsi ilivyo
vyema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja. Ni kama Mafuta mazuri kichwani,
yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. Kama
umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. Maana ndiko BWANA alikoamuru
baraka, Naam, uzima hata milele.
b. Kuwatii
na kuwanyenyekea wenye kuwaongoza. Hakuna mwanafunzi anayefaulu darasani kama siyo
mtiifu na mnyenyekevu. Mambo haya mawili hufungua mlango wa mafanikio kwa Kanisa.
Waebrania 13:17
Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao
wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba
wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
c.
Kanisa litie juhudi sana katika
Maombi. 1 Wathethalonike 5:17 “Ombeni bila kukoma”. Palipo
na maombi panamafanikio makubwa.
MWISHO.
Baada yakujifunza somo hili, naamini kila mtu atawajibika
katika kutumia Karama yake. Wale ambao hawakujua Karama sasa wanaweza kuzitambua
na kuanza kutumika Kanisa.
Bwana alistawishe Kanisa Lake.
Endapo una mwaswali au ushauri, tuma kwa Rev. Daniel Ntebi
rntebi@yahoo.com au
kwa kutumia namba ya simu +255 786 533 028.
No comments:
Post a Comment