Waliofanya ngono barabarani mchana wahukumiwa - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Thursday, 11 November 2021

Waliofanya ngono barabarani mchana wahukumiwa

 


Wanandoa nchini Uganda wamehukumiwa kifungo cha miezi 30 jela baada ya kunaswa kwenye video wakishiriki tendo la ndoa katikati ya barabara inayotumiwa na watu wengi mchana kweupe.


Video ya wapenzi hao wawili ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ambapo baadaye walikamatwa na jeshi la polisi nchini humo na kufikishwa mahakamani. 


Wanandoa hao Paskari Hafashimana (29), na mpenzi wake Colodine Mukamulenzi Muhawenimana (24), walionekana kwenye video hiyo wakifanya tendo hilo kwenye barabara ya Kisoro-Bunagana.


Wakisomewa mashtaka yao wanandoa hao walikubali kutenda kosa hilo na waliomba wapunguziwe adhabu, lakini Hakimu aliamuru wafungwe jela kwa muda wa miezi 30.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here