Serikali ya Ghana imesema kuanzia usiku wa manane siku ya Jumapili wageni wote wanaotembelea nchi hiyo wanahitaji kupewa chanjo kamili dhidi ya Covid 19 kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini humo.
Raia wa Ghana ambao wana nia ya kurejea nchini katika wiki mbili zijazo hawaruhusiwi, lakini watapewa chanjo watakapowasili, taarifa kutoka kwa huduma ya afya ya nchi hiyo inasema.
"Waghana wote wanaosafiri nje ya nchi wanapaswa kupewa chanjo kamili," taarifa hiyo inaongeza.
Agizo hilo ni sehemu ya hatua za kusaidia kudhibiti kuenea kwa aina mpya ya kirusi cha Covid19, Omicron
Taarifa ya huduma ya afya inasema kwamba visa vingi vya kirusi hicho nchini vilitoka kwa watu waliofika katika uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Accra - na wengi wa watu hao walikuwa hawajachanjwa.
Ghana imerekodi zaidi ya visa 130,000 vya Covid 19 kwa jumla na vifo 1,200.
No comments:
Post a Comment