Juventus wamekubali kumsajili mshambuliaji wa Fiorentina na Serbia Dusan Vlahovic, 21, ambaye amekuwa akihusishwa na Arsenal, kwa mkataba wa thamani ya £62.4m. (Mail, via Guardian)
Porto wamekataa ofa ya Tottenham ya pauni milioni 37 pamoja na nyongeza kwa winga wa Colombia Luis Diaz, 25, ambaye ana kipengele cha mkataba cha kuachiliwa kwa pauni milioni 66. (Evening Standard)
Newcastle United wamekamilisha dili la kumsaini kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes, 24, kutoka Lyon kwa pauni milioni 30.(Talksport)
Kocha wa Roma Jose Mourinho ana matumaini kuwa timu hiyo ya Serie A inaweza kumsajili kiungo wa kati wa Arsenal na Uswizi Granit Xhaka, 29, kabla ya dirisha la usajili la Januari kufungwa. (Mail)
Walengwa wawili wakuu wa West Ham katika dirisha la usajili la Januari ni mshambuliaji wa Albania Armando Broja, 20, ambaye yuko kwa mkopo Southampton kutoka Chelsea, na mshambuliaji wa Chile, Ben Brereton Diaz, 22, anayechezea Blackburn Rovers. (Football Insider)
Everton, Leeds United na Wolves pia wana nia ya kumsajili Broja, ambaye Southampton wanataka kumbakisha. (Teamtalk)
Aston Villa wamekataa dau la pauni milioni 30 kutoka kwa klabu ya Ligi ya Primia ambayo haijatajwa jina kwa ajili ya kiungo wa kati wa Brazil Douglas Luiz. Arsenal wanafikiria kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka . (Evening Standard)
Mbio za Arsenal kumnunua Cody Gakpo, 22, zitalazimika kusubiri hadi angalau dirisha la kiangazi kwani PSV Eindhoven wamemfungia Uholanzi kuongeza mkataba. (Mail)
Arsenal wamekubali mkataba wa kumsaini mlinda mlango wa Marekani Matt Turner, 27, kutoka klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya New England Revolution msimu wa joto.(Athletic - subscription required)
Aston Villa, Everton na Leicester City wanamfuatilia mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Jesse Lingard, 29, huku uhamisho wa kiungo mshambuliaji wa Manchester United kwenda Newcastle United ukiporomoka. (Manchester Evening News)
Barcelona wamefanya mawasiliano na Borussia Dortmund huku wakitafuta kumsajili beki wa kulia wa Ubelgiji Thomas Meunier, 30 kwa mkopo . (Marca)
Chelsea ilitoa ofa ya pauni milioni 3 kwa Lyon kama fidia ili kumrejesha mlinzi wa kushoto wa Italia Emerson Palmieri, 27, mapema kutoka kwa mkopo wa muda mrefu katika klabu hiyo ya Ufaransa lakini jaribio hilo lilikataliwa. (Mail, via Athletic)
Ashley Young wa Aston Villa, ambaye anaweza kucheza kama beki au winga, amekataa kuhamia Newcastle United, huku mchezaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 36 akitaka kusalia Villa Park. (Mirror)






No comments:
Post a Comment