Serikali ya Tanzania imeeleza kuwa itakutana na wananchi wanaoishi katika Hifadhi ya Ngorongoro na Loliondo kwa lengo la kuwasikiliza na kuwaelimisha ili kumaliza migongano iliyopo kwenye hifadhi hizo.
Akizungumza bungeni jijini Dodoma Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameagiza viongozi wa serikali yake kukutana na viongozi mbalimbali wa maeneo ya Ngorongoro na wananchi wa eneo hilo ili kumaliza sakata hilo.
No comments:
Post a Comment