Mshambuliaji wa Chelsea Romelu Lukaku amehusishwa na kurejea katika klabu yake ya zamani Inter Milan lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 28 anataka kusalia na kupigania nafasi yake Stamford Bridge. (Mirror)
Manchester City wanaongoza katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland kutoka Borussia Dortmund msimu huu wa joto, wakati Barcelona, Bayern Munich, Paris St-Germain na Real Madrid pia wametoa ofa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. Real wanataka Haaland abaki Dortmund kwa msimu mmoja zaidi kabla ya kumsajili. (SER Deportivos - In Spanish)
Mkurugenzi wa michezo wa Dortmund Hans-Joachim Watzke anatarajia mustakabali wa Haaland katika klabu hiyo ya Ujerumani kuamuliwa katika muda wa wiki sita zijazo. (RTL - in German)
Mkataba wa mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe katika klabu ya Paris St-Germain unamalizika msimu wa joto na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 amekataa ofa nyingine ya kandarasi kutoka kwa timu hiyo ya Ufaransa. (Marca)
Arsenal, Chelsea, Manchester City, Manchester United na Tottenham wanavutiwa na mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 28, ambaye yuko tayari kuondoka Juventus wakati mkataba wake na timu hiyo ya Serie A utakapokamilika msimu wa joto. (90min)
Manchester United wana nia ya kumsajili mlinzi wa kati wa Ujerumani Antonio Rudiger kwa uhamisho wa bure wakati mkataba wake na Chelsea utakapokamilika msimu wa joto na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 atachelewesha uamuzi hadi mwisho wa msimu. (mirror)
Manchester United wana nia ya kumsajili mlinzi Manuel Akanji kutoka Borussia Dortmund na inasemekana tayari wamewasilisha ofa kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi mwenye umri wa miaka 26. (Bild)
Chelsea wamefutilia mbali jaribio la kumnunua winga wa Bayern Munich na Ujerumani Serge Gnabry, 26, na badala yake itamsajili mshambuliaji wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele, 24, msimu wa joto. (Sport - in spanish)
Mshambuliaji wa Watford Ashley Fletcher, 26, anakaribia kujiunga na klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya New York Red Bulls kwa mkopo. (Sun)
Wakala wa mshambuliaji wa Argentina Lautaro Martinez, ambaye amekuwa akihusishwa na Manchester United na Barcelona, anasema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 "anafuraha" katika klabu ya Inter Milan. (FcInternews.it)
Arsenal wamesimamisha mazungumzo kuhusu mustakabali wa mshambuliaji wa Ufaransa Alexandre Lacazette, 30, hadi mwisho wa msimu huu. (Standard)
Newcastle United walishindwa kumnunua mshambuliaji wa Atalanta Duvan Zapata mwezi Januari lakini bado wana nia ya kumsajili mchezaji huyo wa Colombia mwenye umri wa miaka 30. (Football transfers)
Barcelona wanafikiria kumnunua kiungo wa kati Saul Niguez msimu wa joto wakati mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania, 27, anatarajiwa kurejea Atletico Madrid kutoka Chelsea kwa mkopo. (Sport -in spanish)
Real Madrid wana imani kamili na beki wa kulia wa Uhispania Dani Carvajal, 30 na hawana mpango wa kusajili mchezaji mpya katika nafasi yake wakati wa kiangazi. (Marca)
Mshambulizi wa Paris St-Germain na Brazil Neymar, 30, amefichua kuwa alikataa nafasi ya kusajiliwa na Real Madrid akiwa kijana. (Fenomenos podcast, via Goal)






No comments:
Post a Comment