Waziri Mkuu wa Libya anusurika jaribio la mauaji - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Wednesday, 9 February 2022

Waziri Mkuu wa Libya anusurika jaribio la mauaji

 

th

Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid al-Dbeibah amenusurika katika jaribio la mauaji lililofanywa na watu wasiojulikana.

Gari lake lilishambuliwa kwa risasi lilipokuwa likiendeshwa katika mji mkuu, Tripoli, mapema siku ya Alhamisi.

Watu wenye silaha walikimbia eneo la tukio.

Pande zinazozozana zimekuwa zikigombea udhibiti wa Libya, na bunge lenye makao yake mashariki mwa nchi hiyo litapiga kura baadaye siku ya Alhamisi kumchagua waziri mkuu atakayechukua nafasi ya serikali ya umoja wa kitaifa.

Bw Dbeibah amesema kuwa atapuuza matokeo ya kura hiyo.

Uchaguzi wa kuichagua serikali mpya uliahirishwa Disemba mwaka jana lakini hakuna kura inayotarajiwa mwaka huu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here