Mmiliki wa klabu ya Chelsea, Roman Abramovich amewekewa vikwazo na serikali ya Uingereza kama sehemu ya majibu yake kwa uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine.
Yeye ni mmoja wa wafanyabiashara saba matajiri kuwekewa vikwazo vipya, ikiwa ni pamoja na kuzuiliwa kwa mali yao na marufuku ya kusafiri.
Orodha hiyo pia inajumuisha mabilionea Igor Sechin na Oleg Deripaska, wote wanaoonekana kuwa washirika wa Vladimir Putin.
Waziri Mkuu Boris Johnson alisema "hakuwezi kuwa na maeneo salama" kwa wale ambao wameunga mkono uvamizi huo.

No comments:
Post a Comment