Shughuli ya kutafuta ndege iliyokuwa inambeba makamu rais wa Malawi inaendelea - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Tuesday 11 June 2024

Shughuli ya kutafuta ndege iliyokuwa inambeba makamu rais wa Malawi inaendelea

Makamu rais wa Malawi, Saulos Chilima
Makamu rais wa Malawi, Saulos Chilima

Shughuli za kutafuta na za uokoaji zitaendelea hadi ndege iliyopotea iliyokuwa inambeba makamu rais wa Malawi Saulos Klaus Chilima, ipatikane, rais wa taifa hilo la Kusini mwa Afrika alisema Jumatatu.

Chilima alikuwa ndani ya ndege ya kijeshi na watu wengine tisa ilipoondoka mjini Lilongwe nyakati za asubuhi, ofisi ya Rais wa Malawi ilisema katika taarifa ya awali.

Ilisema juhudi za mamlaka ya usafiri wa anga kuwasiliana na ndege hiyo tangu ilipopotea kwenye mitambo ya rada hazikufaulu. Ndege hiyo ilitarajiwa kutua kwenye uwanja wa ndege wa Mzuzu saa nne asubuhi majira ya huko.

Ndege hiyo haikuweza kutua kwenye uwanja huo kutokana na hali mbaya ya hewa na kuamriwa kurejea katika mji mkuu, Rais Lazarius Chakwera alisema katika hotuba yake kwa taifa kwa njia ya televisheni.

“Ninayo matumaini kwamba tutawapata manusura,” alisema, akiongeza kuwa shughuli za kuitafuta ndege hiyo zimejikita karibu na eneo la kilomita 10 katika hifadhi ya msitu.

“Nimetoa maagizo kamili kwamba shughuli hiyo iendelee hadi ndege ipatikane,” alisema.

Alisema Malawi iliwasiliana na nchi jirani, na serikali za Marekani, Uingereza, Norway na Israel kusaidia katika juhudi za ukoaji.


     

    No comments:

    Post a Comment

    Post Top Ad

    Responsive Ads Here