Mtendaji Mkuu wa Benki ya Absa wa Afrika Mshariki, Bw. Saviour Chibiya (wa tatu kutoka kulia), akiwa katika mazungumzo na Bw. Rumisho Shikonyi (wa tatu kutoka kushoto), Meneja Mkazi wa taasisi ya kifedha ya Watu Credit Tanzania, alipofanya ziara katika taasisi hiyo, jijini Dar es Salaam jana, akiambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kutoka kulia), pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo. Mazungumzo yao yalilenga kuimarisha ushirikiano, kufungua fursa mpya, na kuendeleza ukuaji endelevu. Bw. Chibiya kwa sasa yupo Tanzania kwa ziara yake rasmi ya kikazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), akizungumza na Bw. Rumisho Shikonyi (kulia), Meneja Mkazi wa taaisis ya Watu Credit Tanzania, wakati Mtendaji Mkuu wa Benki ya Absa wa Afrika Mashariki, Bw. Saviour Chibiya (wa pili kutoka kushoto), akifanya ziara katika kampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mazungumzo yao yalilenga katika kuimarisha ushirikiano, kufungua fursa mpya, na kuendeleza ukuaji endelevu. Bw. Chibiya kwa sasa yupo Tanzania kwa ziara yake rasmi ya kikazi. Kushoto ni Ofisa Fedha Mkuu wa Absa Bank Tanzania, Bw. Bernard Tesha.
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Absa wa Afrika Mashariki, Bw. Saviour Chibiya (kushoto), akimsikiliza kwa makini Bw. Rumisho Shikonyi (kulia), Meneja Mkazi wa taasisi ya Watu Credit Tanzania, wakati wa ziara yake katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam jana. Alifuatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kusoto kwake), pamoja na viongozi wengine waandamizi wa benki hiyo. Mazungumzo yao yalilenga katika kuimarisha ushirikiano, kufungua fursa mpya, na kuendeleza ukuaji endelevu. Bw. Chibiya kwa sasa yupo Tanzania katika ziara yake rasmi ya kikazi.
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Absa wa Afrika Mashariki, Bw. Saviour Chibiya (wa tatu kushoto), Bw. Obedi Laiser (wa pili kutoka kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania; na Bw. Rumisho Shikonyi (wa nne kutoka kushoto), Meneja Mkazi wa Watu Credit Tanzania, wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na maafisa waandamizi kutoka taasisi zote mbili baada ya ziara ya Bw. Chibiya katika taasisi hiyo ya fedha, jijini Dar es Salaam jana.
No comments:
Post a Comment