![]() |
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)wametajwa kuwa ni maadui ambao watapelekea chama hicho kukosa ushindi katika chaguzi mbili zijazo.
Akifungua mkutano wa ndani wa Baraza la uongozi la CHADEMA Kanda ya Pwani, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amesema kuwa, maadui wa chama hicho ni baadhi ya wanachama wanaoweka maslahi binafsi mbele kuliko ya Chama na ya wananchi wanaofifisha jitihada za kukijenga.
“Umefika wakati kwa wanachama wetu kufikiria masilahi mapana ya wananchi na chama la sivyo itakuwa vigumu kushika dola, na kama wanachama watajikita kutetea masilahi binafsi kama ilivyotokea kwa baadhi, ni dhahiri lengo la kuongoza nchi halitafikiwa“, amesema Sumaye.
Sunaye ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho baadhi ya wabunge, madiwani, wenyeviti wa halmashauri na wanachama wakijiuzulu nafasi zao na kutimkia CCM ambako baadhi yao walipitishwa na kurudi kwenye nyadhifa hizo.
Uchaguzi wa serikali za mitaa nchini unatarajiwa kufanyika mwakani kabla ya uchaguzi mkuu 2020.
|
Wednesday, 19 December 2018
Sumaye awaanika maadui wa Chadema
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
No comments:
Post a Comment