Rwanda yapiga marufuku vyombo vya plastiki vinavyotumiwa mara moja - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Tuesday, 22 October 2019

Rwanda yapiga marufuku vyombo vya plastiki vinavyotumiwa mara moja

Wizara ya mazingira ya Rwanda imetangaza kupiga marufuku vyombo vya plastiki  ambavyo vinatumiwa mara moja na kurejelezwa.

Ni miaka  10 tangu serikali ya Rwanda kupiga marufuku  katika ukanda wa Afrika Mashariki matumizi ya mifuko ya plastiki kwa lengo la kulinda mazingira.

Wizara ya mazingira chini ya uongozi wa waziri Vincent Biruta imetangaza sheria mpya ambayo inapiga marufuku  matumizi ya  vyombo na bidhaa za plastiki ambazo hutumiwa mara moja na kurejelezwa.

Waziri wa mazingira wa Rwanda amenukuliwa na vyombo vya habari nchini Rwanda  akitoa muda wa miezi  mitatu  kwa wafanya  biashara wa bidhaa za plastiki kuwa wawe wamekwishasitisha  biashara hiyo.

Sheria hiyo ina lenga bidaa za plastiki kama  vikombe,  masahani, mirija ya vinywaji na bidhaa nyingine ambazo ni za plastiki.

Adhabu kweli itatolewa kwa mtu yeyote atakaekwenda kinyume na sheria.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here