Mwisho wa Twitter ujumbe, 1

Lewandowski aliibiwa?

Wakosoaji wengine wanafikiri kuwa mshambulizi wa Bayern Munich na Poland Lewandowski aliyemaliza nafasi ya pili alistahili kushinda tuzo hiyo.

Mchezaji huyu mwenye miaka 33 alifunga mabao 53 katika mashindano yote kwa Bayern mwaka 2021 na alishinda tuzo la mshambulizi wa mwaka.

Mwaka uliopita tuzo za Ballon d'Or zilifutwa kwa sababu ya janga lakini wengi walihisi angetambuliwa kwa njia nzuri wakati huo, baada ya kipindi kizuri ambapo aliisaidia Bayern kupata mataji matatu, la Ligi kuu, Bundelsiga na la Ujerumani la DFB

Mwaka 2021 Bayern ilijiongezea kombe lingine la Bendelsiga na kushinda mara ya tisa mfululizo ambapo Lewi alivunja rekodi ya sogora Gerd Muller's ya mabao 41 katika Bendesliga kwa msimu mmoja

Ruka Twitter ujumbe, 2

Mwisho wa Twitter ujumbe, 2

Ruka Twitter ujumbe, 3

Mwisho wa Twitter ujumbe, 3

Kiungo wa kati wa Real Madrid Toni Kroos hakukubaliana kabisa na uamuzi aa kumpa Messi nafasi ya kwanza

Alisema , hakuna shaka kuwa Messi na Cristiano wamekuwa wachezaji wa muongo uliopita, lakini mwaka huu kuna wengine mbele yake.

Kroos aliwataja wachezaji bora watatu kama mwenzake wa Real Madrid Karim Benzema, Lewandowski na Jorginho.

Sogora wa Real Madrid Casilla aliingilia kati pia akisema, "ni vigumu sana kwangu kuamini tuzo za soka. Messi ni kati ya wachezaji bora lakini ni lazima ujue ni nani bora zaidi baada ya msimu, sio vigumu."

Sio kila mtu ana chuki

Baada ya hayo yote kusemwa, kulikuwa na uungwaji mkono mwingi kwa uamuzi wa kumtambua Messi tena.

Ruka Twitter ujumbe, 4

Mwisho wa Twitter ujumbe, 4

Ruka Twitter ujumbe, 5

Mwisho wa Twitter ujumbe, 5

Ruka Twitter ujumbe, 6

Mwisho wa Twitter ujumbe, 6

Jorgino alistahili kuwa katika nafasi kwanza tatu?

Kiungo wa safu ya kati wa Chelsea raia wa Italia Jorginho alishika nafasi ya tatu naye mchezaji mwenzake N'Golo Kante akashika nafasi ya tano.

Ruka Twitter ujumbe, 7

Mwisho wa Twitter ujumbe, 7

Ruka Twitter ujumbe, 8

Mwisho wa Twitter ujumbe, 8

Ruka Twitter ujumbe, 9

Mwisho wa Twitter ujumbe, 9

Na hata hivyo bado ana wapinzani wake

Ruka Twitter ujumbe, 10

Mwisho wa Twitter ujumbe, 10

Lionel Messi na Robert Lewandowski katika tuzo za Ballon d'Or

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Mashabiki wa Lewindowski wanasema kwamba alipokonywa ushindi

Kipi kilimpata Mohamed Salah?

Salah ametajwa kuwa mchezaji bora zaidi duniani na wachambuzi kadhaa msimu huu na meneja wake huko Liverpool Jurgen Klopp. Lakini alimaliza nafasi ya saba kwenye kura ya tuzo za Ballon d'Or nafasi moja nyuma ya Cristiano Ronaldo.

Ruka Twitter ujumbe, 11

Mwisho wa Twitter ujumbe, 11

Ruka Twitter ujumbe, 12

Mwisho wa Twitter ujumbe, 12

Klopp akishangzwa kuwa raia huyo wa Misri hakupta kura zaidi.

"Kwa uhakika Mo angekwa nafasi nzuri," alisema Mjerumani huyo na kuvilaumu vyombo vya habari.

Klopp alihoji kukosekana kwake Lewandowski.

"Unaweza kumpa Lionel Messi tuzu kwa taaluma amekuwa nayo, na mabao haya yote lakini usimpe Lewandowski wakati huu - kwa hivyo ni vigumu kuishinda kabisa."

Je, wanawake walipuuzwa?

Ukosoaji mwingine ulihusu uamuzi wa kuandaa tuzo hizo wakati wa mapumziko ya kimataifa kutoka soka ya wanawake, ikimaanisha kuwa wachezaji wengine bora hawakuweza kuhudhuria.

Ruka Twitter ujumbe, 13

Mwisho wa Twitter ujumbe, 13

Ruka Twitter ujumbe, 14

Mwisho wa Twitter ujumbe, 14

Pia mchezaji wa kimataaifa wa Canada Stephanie Labbe hakuwa makini kuhusu Ronaldo kutajwa kuwa mfunganji bora wa kimataifa wakati wa sherehe. Mchezaji mwenzake Christine Sinclair anashikilia rekodi hiyo na mabao 188 kwa Canada.

Ni mwishowe….

Nani aliamua ilikuwa wazo zuri kuonyesha picha hii ya Ronaldo?

Ruka Twitter ujumbe, 15

Mwisho wa Twitter ujumbe, 15

Picha ya Didier Drogba na Cristiano Ronaldo picha ya pili ni ya Robert Lewandowski na Lionel Messi wakitabasamu.

CHANZO CHA PICHA,@RONALDOCOMPS

Maelezo ya picha,

Picha ya Didier Drogba na Cristiano Ronaldo picha ya pili ni ya Robert Lewandowski na Lionel Messi wakitabasamu.

Tunahisi kuwa Twitter haitapata amani kwa muda kufuatia matokeo ya mwaka huu ya tuzo za Ballon d'Or…