Wabunge nchini Mali kwa kauli moja wameidhinisha mpango wa kuruhusu utawala wa kijeshi wa kipindi kisichozidi miaka mitano.
Mpaka sasa hakuna tarehe iliyowekwa kwa ajili ya uchaguzi uajo.
Uchaguzi mkuu nchini humo ulitarajiwa kufanyika mwezi uliopita lakini ulifutwa na viongozi wa kijeshi wa Mali, na kusababisha vikwazo vya kiuchumi kutoka Jumuiya ya kikanda, ECOWAS.
Kwa sasa Mali inachukua hatua za kisheria kuondoa vikwazo vilivyowekwa na muungano wa fedha wa Afrika Magharibi, Uemoa, wakati huu ikipambana kukabiliana na madeni makubwa.

No comments:
Post a Comment