Timu zinazotegua mabomu nchini Lebanon zinahitaji kuvaa vifaa vizito vya kujikinga na kuanza kazi yao mapema ili kuepusha hali ya joto.
Kutembelea eneo lenye vilipuzi kunaanza na tahadhari muhimu ya usalama. Na itaokoa maisha yako - wakati uko mbali kidogo na vilipuzi vilivyozikwa, unahitaji kuwa makini.
Vijiti vya rangi nyekundu vilivyochimbwa chini vinamaanisha hatari. Sogea zaidi na una hatari ya kukanyaga kilipuzi. Vijiti vyeupe ni ishara ya njia salama, iliyosafishwa. Vijiti vyeusi vinaonyesha mahali kilipuzi kilikuwa kimezikwa, na vilipuzi vilivyokuwa ndani sasa vimeharibiwa.
Kuvaa vifaa vya kujinga ni muhimu. Hiyo inamaanisha kofia inayofunika uso wako kutoka sikio hadi sikio na kufunika chini ya kidevu. Mavazi ya kujinga mwili hufika karibu na magoti yako, kukinga viungo na mishipa yako muhimu dhidi ya athari ya mlipuko wowote wa bahati mbaya.
Joto la kiangazi nchini Lebanon, linadhoofisha. Walipua vilipuzi huanza kazi yao mara tu jua linapochomoza, ili kupata baridi zaidi. Kila saa huchukua dakika 10 kupumzika. Jua la adhuhuri linapofika hatua yake ya juu zaidi wanakaribia kumaliza kazi ya siku hiyo.
Ni hatari sana kufanya kazi wakati hali inamaanisha unaweza kupoteza umakini. Hata kuteleza kidogo kunaweza kusababisha kifo.
Ilikuwa miaka 25 iliyopita mwezi huu, tarehe 3 Desemba 1977, ambapo mkataba wa Ottawa ulitiwa saini. Unajulikana zaidi kama Mkataba wa Kupiga Marufuku Vilipuzi - makubaliano ya kimataifa ambayo yalipiga marufuku mabomu ya ardhini - na inachukuliwa kuwa mojawapo ya mikataba iliyofanikiwa zaidi ya upokonyaji silaha duniani. Hadi sasa, nchi 164 zimekubali kujiunga nayo.
Wiki chache kabla ya mkataba huo kutiwa saini, Kikundi cha Ushauri wa Vilipuzi (MAG) kilishinda Tuzo ya Amani ya Nobel kwa juhudi zao za kuchukua hatua za vilipuzi kote ulimwenguni.
Wamekuwa wakifanya kazi nchini Lebanon tangu 2001. Operesheni ya kutegua mabomu ni kubwa na inaendelea karibu kila siku. Mwaka huu pekee watasafisha mita za mraba milioni mbili za ardhi na kuharibu karibu mabomu 10,000 ya ardhini.
Wafanyakazi wanaofanya kazi na Kikundi cha Ushauri wa Migodi (MAG) wamefanikiwa kuharibu mabomu 10,000 mwaka huu pekee.
Pamoja na kushughulika na mabomu katika Bonde la Bekaa na vilipuzi vilivyoboreshwa (IEDs) vilivyoachwa na kundi la Islamic State (IS) kaskazini-mashariki mwa nchi, kazi kuu inahusisha kutegua mpaka kati ya Lebanon na Israel.
Kinachojulikana kama Blue Line kilichorwa na Umoja wa Mataifa mnamo 2000, iliyoundwa kuashiria uondoaji wa vikosi vya Israeli kutoka kusini mwa Lebanon. Katika sehemu fulani ni ukuta mrefu, katika nyingine ni zaidi ya ua wa chuma ambao unaweza kuuona.
Chini kuna ardhi ya urefu wa kilomita 120 (maili 75) yenye vilipuzi isiweza kupenyeka. Takriban vilipuzi 400,000 viliwekwa hapo, baadhi yao vikiwa umbali wa mita moja kati yao.
Katika kijiji cha Arab Ellouaizi, kizuizi kinachoashiria mwisho wa Lebanon na kuanza kwa Israeli kiko kwenye ukingo wa eneo lenye vilipuzi. Mita moja au mbili mbali mnara wa kijeshi wa Israeli unaonekana nyuma ya matofali vu. Vilima vilivyo mbali vimefunikwa na ukungu.
Ardhi hii yenye vilipuzi vingi ni tatizo hatari kwa idadi kubwa ya wakimbizi waliokuja Lebanon kutoka Syria. Wanataka kuishi kwenye ardhi, na kuilima, lakini hawajui hatari zake.
Robo tatu ya wakazi wa Arab Ellouaizi ni wakimbizi wa Syria wanaojaribu kutafuta riziki mamia ya maili kutoka nyumbani. Na ndio maana kuna sababu nyingine muhimu - mbali na usalama - kusafisha eneo hili.
Kilimo ndio kazi kuu katika kusini, na wakulima wanatamani sana kusafishwa kwa ardhi ili waweze kuitumia. Mgogoro wa kifedha wa Lebanon, pamoja na uhaba wa chakula unaosababishwa na vita nchini Ukraine, inamaanisha kuwa kilimo ni kipaumbele cha dharura.
Wakulima katika eneo hilo wanatamani kusafishwa ardhi yao ili waweze kulima mazao ya kusaidia kukabiliana na uhaba wa chakula.
Abu Ghassan Awada ana zao la pilipili lililo nono na tayari kuvunwa. Juu yao, miti ya peach hufikia juu ya vichwa vyetu. Anakumbuka sauti ya milipuko usiku wakati mbuzi, kondoo na mbweha walipoenda kwa vilipuzi. Ilimaanisha kwamba kwa miaka mingi, hangeweza kulima ardhi yake.
"Nilikuwa mfanyakazi tu, kuajiriwa na watu wengine. Lakini sasa ninaweza kuajiri watu wa kufanya kazi kwenye kiwanja changu," anasema.
Bado huchukua muda kutunza na kurekebisha uawa chuma unaoonyesha ukingo wa shamba lake. Zaidi ya hayo, umbali wa mita chache tu, ardhi bado ina vilipuzi.
Baadhi ya wafanyikazi waliohudumu kwa muda mrefu zaidi wa MAG wamekuwa sehemu ya timu kwa miongo kadhaa. Bango kubwa kwenye mlango wa makao yao makuu linaonyesha majina na nyuso zao. Hiba Ghandour ni meneja wa programu wa MAG nchini Lebanon.
Pia ana shauku ya kuhakikisha kuwa wanawake wengi kama wanaume wanahusika katika kazi ya kutegua mabomu. "Tunapotangaza kazi ambazo tunapaswa kujaza, hata kuongeza picha ya mwanamke anayefanya kazi hiyo inahakikisha kuwa tunaweza kumfikia kila mtu," aeleza.
Mmoja wa wanawake hao ni Suaad Hoteit. Alianza kazi hiyo miaka minne iliyopita, na hata alikutana na mchumba wake walipokuwa wakifanya kazi pamoja katika uwanja wa migodi.
Akivuta kofia yake kichwani kwa ustadi, anaelezea kazi ya siku hiyo. "Ninachukua detector yangu, kisha naenda shambani na kuanza kupekua. Nikipata kilipuzi, nampigia simu msimamizi kuangalia. Na mwisho wa siku, ninakilipua."
Suaad Hoteit alianza kazi migodini miaka minne iliyopita, na hata alikutana na mchumba wake walipokuwa wakifanya kazi pamoja huko.
Ninashangazwa na jinsi anavyozungumza juu ya jambo hatari sana. "Ni miaka minne sasa, kwa hivyo ni utaratibu wa kila siku," anatabasamu. "Katika mwaka wa kwanza wa kuwa hapa, niliogopa sana. Sasa ninaelewa hatari. Na ninafanya kazi hapa kwa sababu ninataka kuwaonyesha watu kwamba wanawake wanaweza kufanya chochote. Tuna nguvu na tunajitegemea."
Aina ya mabomu ya ardhini ambayo Suaad anayatafuta bado yanajeruhi na kuua watu mara kwa mara katika nchi 60 tofauti. Ulimwenguni kote, kuna karibu majeruhi 15 kila siku. Haidar Maarouf Haidar alikuwa mmoja wao.
Anavaa kiegemeo maalum cheupe chenye elastic kwenye mkono wake wa kulia, na kuivua kwa uangalifu anapokumbuka siku alipolipua kilipuzi akipanda miti kwenye bustani yake. Wakati bado uko katika kumbukumbu yake, ingawa ilitokea miaka miwili iliyopita.
“Ghafla kitu kililipuka na nikasikia sauti kana kwamba nilikuwa ndotoni, sikujua nini kimetokea, muda mmoja nikiwa nimeinama chini ghafla kitu kilinishika, nilipigwa na kupoteza fahamu na nilipoamka sikuweza kuona vidole vyangu. Vilikuwa vimeondoka."
Haidar anageuza mkono wake kunionyesha vidole vilivyosalia - visiki vinne tu vinavyosokota kutoka kwenye kiganja. "Hali yangu ya kisaikolojia imebadilika, ndio kwanza nilikuwa mfanyakazi wa kila siku, nilikuwa nafanya kila kitu kwa mikono yangu, kuvunja mawe na mbao.
Mwili wangu ulikuwa hai, sasa nikitumia mikono yangu najisikia kama umeme ndani yao. Majeraha yangu ya mguu yanafanya iwe vigumu kutembea. Maisha yangu yamebadilika kabisa, siwezi kufanya kazi yoyote tena isipokuwa kulea watoto wangu."
Haidar Maarouf Haidar alipoteza sehemu za vidole vyake kwa mkono mmoja wakati mgodi ulipolipuka alipokuwa akipanda miti kwenye bustani yake.
Baada ya maumivu makali sasa mstari wa kumalizia unaonekana - angalau huko Lebanon. Tunaposimama pamoja katika eneo la vilipuzi la Arab Ellouaizi, Hiba Ghandour wa MAG anataka kubainisha wamefikia wapi.
"Kwa ujumla nchini Lebanon tumesafisha 80% ya ardhi iliyochafuliwa. Tunahitaji tu kuendelea, na ni msaada wa wafadhili wetu wa kimataifa ambao unawezesha."
Nchi kama Marekani, Ufaransa, Norway, Uholanzi na Japan ziko mstari wa mbele katika ufadhili wa uchimbaji vilipuzi. Msaada ni muhimu, lakini kiasi cha pesa kilichoahaidiwa kinapungua. Nchini Lebanon pekee kimeshuka kutoka $19.7m (£16m) mwaka 2019 hadi $12.1m kinachotarajiwa mwaka 2023.
Ni vigumu kutabiri itachukua muda gani kusafisha asilimia 20 iliyobaki ya ardhi iliyochafuliwa ya Lebanon. Kubadilika kwa ufadhili ni sababu moja. Lakini teknolojia mpya huchukua sehemu kubwa katika wakati pia. Katika mwaka jana mashine udongo na vifaa vyake vilivyofichwa, ikizivunja vipande-vipande kabla ya kulipuka.
Wakati mwingine hulipua ndani ya mashine. Haichukui nafasi ya wachimbaji wananadamu, kwa sababu inaweza tu kufanya kazi kwenye eneo tambarare. Lakini hakika hufanya kazi iwe haraka.
Baadhi ya vilipuzi vikubwa pia vinashughulikiwa kwa njia mpya na maalum. Timu za kutegua mabomu sasa ziko karibu sana na mpaka unaoathiriwa na siasa kati ya Lebanon na Israel kiasi kwamba kulipua vilipuzi hivyo vikubwa kunahatarisha kuharibu mpaka.
Hilo halitakuwa zuri kwa uhusiano dhaifu kati ya nchi hizo mbili. Kwa hiyo sasa, vijiti maalum vya thermite vinaingizwa kwenye vilipizi kwenye ardhi. Joto kali huchoma vilipuzi bila kuleta mlipuko mkubwa.
Mbele ya miali ya moto mkali Mohammed Atris anabembeleza machipukizi ya kijani kibichi yanayofunika ardhi yake. Kwa miongo kadhaa ardhi anayomiliki imekuwa haitumiki, imejaa vilipuzi. Hata kutembea juu yake ilikuwa hatari. "Nilihisi huzuni, huzuni na kuchanganyikiwa," anasema.
"Siwezi kuelezea hisia za kutoweza kutumia ardhi ambayo tulikulia hapo awali katika maisha yetu kabla ya kuchimbwa na kufanywa kutofaa kwa kilimo. Ilikuwa mbaya sana."
Mboga anazotunza zilipandwa wiki sita tu zilizopita, saa 24 pekee baada ya shamba hilo kutangazwa kuwa safi na kukabidhiwa kwake.
"Sikuweza kusubiri. Kwa wote waliofanikisha hili, tunawashukuru kwa jitihada zenu."
Akiwa ameinama ili kung'oa mazao yake mapya, anafuta udongo kwa upole kutoka kwenye mizizi yake na kutabasamu.






No comments:
Post a Comment