Makamu wa Rais kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Umoja wa Mataifa (UN) - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Thursday 19 October 2017

Makamu wa Rais kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Umoja wa Mataifa (UN)


Makamu wa Rais kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Umoja wa Mataifa (UN)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 72 ya umoja wa Mataifa UN yanayotarajiwa kufanyika Oktoba 24 mwaka huu katika ukumbi wa Kareemjee jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini humo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Susan Kolimba amesema kuwa zaidi ya watu 500 wanatarajiwa kushiriki katika maadhimisho hayo wakiwemo watumishi wa Serikali,mabalozi wa nchi mbalimbali,wanafunzi,vyombo vya Usalama ,wadau mbalimbali pamoja na wananchi walioalikwa kuhudhuria katika siku hiyo.

Pia amesema kuwa UN kwa kupitia Taasisi zake wameweza kutoa misaada mbalimbali hapa nchini ikiwa ni pamoja na kutoa dollar za kimarekani laki 1 sawa na Milioni 220 za kitanzania katika chuo cha Polisi Moshi ili kuwajengea uwezo walimu kuweza kupambana na ukatili kwa wanawake na Watoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa UN nchini ALVARO RODRIGUEZ amesema kuwa wataendelea kufanya kazi kwa pamoja na Serikali ya Tanzania pamoja na wadau wa maendeleo ili kuweza kuleta maendeleo hapa nchini.

Mbali na maadhimisho hayo kufanyika jijini Dar es salaam lakini pia yatafanyika Zanzibar Oktoba 26 mwaka huu katika hotel ya Serena na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na Kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here