Nape amtahadharisha Lissu na jambo hili baada ya kuongea jana kwa mara ya kwanza - KABATA

This is the special room for news where you need to settle with!


Breaking

Thursday 19 October 2017

Nape amtahadharisha Lissu na jambo hili baada ya kuongea jana kwa mara ya kwanza

Nape amtahadharisha Lissu na jambo hili baada ya kuongea jana kwa mara ya kwanza
bunge wa jimbo la Mtama kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Nnauye amefunguka na kusema amefurahi kumuona Tundu Lissu akiwa katika furaha na tabasamu na kumuomba kwa sasa asiseme lolote mpaka pale atakapona kabisaa. 
 
Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema tabasamu la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa kwenye hospitali jijini Nairobi linatoa matumaini makubwa. 
"Mjomba tunamshukuru Mungu kwa tabasamu hili la matumaini!Nakuombea afya iimarike kabla hujasema mengi! Tulia mjomba upone kabisa kwanza" alisema Nape Nnauye 

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma nyumbani kwake na baadaye alipelekwa jijini Nairobi kwa matibabu zaidi ambapo mpka sasa anapatiwa matibabu huko.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here